((وَجَّهْتُ وَجْهِيَ لِلَّذِي فَطَرَ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضَ حَنِيفَاً وَمَا أَنَا مِنَ الْمُشْرِكِينَ، إِنَّ صَلاَتِي، وَنُسُكِي، وَمَحْيَايَ، وَمَمَاتِي لِلَّهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ، لاَ شَرِيكَ لَهُ وَبِذَلِكَ أُمِرْتُ وَأَنَا مِنَ الْمُسْلِمِينَ. اللَّهُمَّ أَنْتَ المَلِكُ لاَ إِلَهَ إِلاَّ أَنْتَ، أَنْتَ رَبِّي وَأَنَا عَبْدُكَ، ظَلَمْتُ نَفْسِي وَاعْتَرَفْتُ بِذَنْبِي فَاغْفِرْ لِي ذُنُوبي جَمِيعَاً إِنَّهُ لاَ يَغْفِرُ الذُّنوبَ إِلاَّ أَنْتَ. وَاهْدِنِي لِأَحْسَنِ الأَخْلاقِ لاَ يَهْدِي لِأَحْسَنِها إِلاَّ أَنْتَ، وَاصْرِفْ عَنِّي سَيِّئَهَا، لاَ يَصْرِفُ عَنِّي سَيِّئَهَا إِلاَّ أَنْتَ، لَبَّيْكَ وَسَعْدَيْكَ، وَالخَيْرُ كُلُّهُ بِيَـــــــدَيْكَ، وَالشَّـــــرُّ لَيْسَ إِلَيْــــــكَ، أَنَا بِكَ وَإِلَيْكَ، تَبارَكْتَ وَتَعَالَيْتَ، أَسْتَغْفِرُكَ وَأَتوبُ إِلَيْكَ)).
Nimeuelekeza uso wangu kwa yule ambae ameumba mbingu na ardhi hali ya kumtakasia yeye dini yangu, na sikuwa mimi ni katika washirikina, hakika swala yangu na kuchinja kwangu na uhai wangu na kufa kwangu ni kwa Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe vyote, hana mshirika, na kwa hilo nimeamrishwa, nami ni katika waislamu, Ewe Mwenyezi Mungu, wewe ndie mfalme, hapana Mola apasae kuabudiwa kwa haki isipokuwa wewe, wewe ndie Mola wangu na mimi ni mja wako, nimeidhulumu nafsi yangu, na nimekiri madhambi yangu kwa hivyo nisamehe madhambi yangu yote, hakika hakuna mwenye kusamehe madhambi isipokuwa wewe, na niongoze katika tabia njema (nzuri) kwani hakuna mwenye kuongoza katika tabia nzuri isipokuwa wewe, niepushe na tabia mbaya, kwani hakuna mwenye uwezo wa kuniepusha na tabia mbaya isipokuwa wewe, naitikia wito wako, na shari haitoki kwako, mimi nimepatikana kwa ajili yako, na nitarudi kwako, umetakasika na umetukuka, nakutaka msamaha na ninarejea kwako (kwa kutubia)
Sikiliza · Sauti ya Hamad al-Duraiham