((اللَّهُ أَكْبَرُ، اللَّهُ أَعَزُّ مِنْ خَلْقِهِ جَمِيعاً، اللَّهُ أَعَزُّ مِمَّا أَخَافُ وَأَحْذَرُ، أَعُوذُ بِاللَّهِ الَّذِي لاَ إِلَهَ إِلاَّ هُوَ، الْمُمْسِكِ السَّمَوَاتِ السَّبْعِ أَنْ يَقَعْنَ عَلَى الْأَرْضِ إِلاَّ بِإِذْنِهِ، مِنْ شَرِّ عَبْدِكَ فُلاَنٍ، وَجُنُودِهِ وَأَتْبَاعِهِ وَأَشْيَاعِهِ، مِنْ الْجِنِّ وَالإِنْسِ، اللَّهُمَّ كُنْ لِي جَاراً مِنْ شَرِّهِمْ، جَلَّ ثَنَاؤُكَ وَعَزَّ جَارُكَ، وَتَبَارَكَ اسْمُكَ، وَلاَ إِلَهَ غَيْرُكَ)) (ثلاثَ مرَّاتٍ).
Mwenyezi Mungu ni mkubwa, Mwenyezi Mungu ni mwenye nguvu (cheo) kuliko viumbe wake wote, Mwenyezi Mungu ni mwenye nguvu, kuliko kila nikiogopacho na kujihadhari, najikinga kwa Mwenyezi Mungu ambae hapana mola ila Yeye tu, ambae ameshikilia mbingu saba, ili zisiangukie ardhi, ila kwa idhini yake, kutokana na shari ya mja wako fulani, na majeshi yake, na wanaomfuata, na wafuasi wake, miongoni mwa majini na watu. Ewe Mwenyezi Mungu, kuwa mlinzi wangu kutokana na shari yao, zimetukuka sifa zako, na umeheshimika ulinzi wako, na limetakasika jina lako, na hapana apasae kuabudiwa kwa haki asiyekuwa Wewe.
Sikiliza · Sauti ya Hamad al-Duraiham