((اللَّهُمَّ لَكَ الْحَمْدُ، أَنْتَ نُورُ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضِ وَمَنْ فِيهِنَّ، وَلَكَ الْحَمْدُ أَنْتَ قَيِّمُ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضِ وَمَنْ فِيهِنَّ، [وَلَكَ الْحَمْدُ أَنْتَ رَبُّ السَّمَواتِ وَالأَرْضِ وَمَنْ فِيهِنَّ] [وَلَكَ الْحَمْدُ لَكَ مُلْكُ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضِ وَمَنْ فِيهِنَّ] [وَلَكَ الْحَمْدُ أَنْتَ مَلِكُ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضِ] [وَلَكَ الْحَمْدُ] [أَنْتَ الْحَقُّ، وَوَعْدُكَ الْحَقُّ، وَقَوْلُكَ الْحَقُّ، وَلِقاؤُكَ الْحَقُّ، وَالْجَنَّةُ حَقٌّ، وَالنَّارُ حَقٌّ، وَالنَّبِيُّونَ حَقٌّ، وَمحَمَّدٌ صلى الله عليه وسلم حَقٌّ، وَالسّاعَةُ حَقٌّ] [اللَّهُمَّ لَكَ أَسْلَمتُ، وَعَلَيْكَ تَوَكَّلْتُ، وَبِكَ آمَنْتُ، وَإِلَيْكَ أَنَبْتُ، وَبِكَ خاصَمْتُ، وَإِلَيْكَ حاكَمْتُ. فَاغْفِرْ لِي مَا قَدَّمْتُ، وَمَا أَخَّرْتُ، وَمَا أَسْرَرْتُ، وَمَا أَعْلَنْتُ] [وَمَا أَنْتَ أَعْلَمُ بِهِ مِنِّي] [أَنْتَ المُقَدِّمُ، وَأَنْتَ المُؤَخِّرُ لاَ إِلَهَ إِلاَّ أَنْتَ] [أَنْتَ إِلَهِي لاَ إِلَهَ إِلاَّ أَنْتَ] [وَلاَ حَوْلَ وَلاَ قُوَّةَ إِلاَّ بِاللَّهِ])).
Mtume (s.a.w) alikuwa akiamka usiku ili kufanya ibada anasema: Ewe Mwenyezi Mungu ni zako sifa njema, Wewe ndie nuru ya mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake, na ni zako sifa njema wewe ndie sababu ya kusimama kwa mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake, na ni zako sifa njema wewe ndiwe Mola wa mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake, na ni zako sifa njema, ni wako ufalme wa mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake, na ni zako sifa njema wewe ndiwe Mfalme wa mbingu na ardhi, na ni zako sifa njema wewe ni Haki (Kweli), na ahadi yako ni ya kweli na neno lako ni lakweli, na kukutana na wewe ni kweli, na pepo ni kweli, na moto ni kweli, na Mitume ni kweli, na Muhammad ni kweli, na Qiyama ni kweli, Ewe Mwenyezi Mungu, kwako nimejisalimisha, na kwako nimetegemea, na wewe nimekuamini, na kwako nimeregea, na kwa ajili yako nimeteta, na kwako nimehukumu, kwahivyo nisamehe niliyoyatanguliza, na niliyo yachelewesha, na niliyo yaficha, na niliyo yatangaza, Wewe ndie mwnye kuchelewesha, hapana Mola apasae kuabudiwa kwa haki isipokuwa wewe.
Sikiliza · Sauti ya Hamad al-Duraiham