MwanzoDhikriFadhila za tasbiih, tahmiid, tahliil na takbiirdhikri 9

Fadhila za tasbiih, tahmiid, tahliil na takbiir — dhikri 9

فضل التسبيح و التحميد، و التهليل، و التكبير · Hisnul Muslim · 9 / 12

Soma · SikilizaFaili la PDF

جَاءَ أَعْرَابِيٌّ إِلَى رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ: عَلِّمْنِي كَلاماً أَقُولُهُ: قَالَ: ((قُلْ: لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ وَحْدَهُ لاَ شَرِيكَ لَهُ، اللَّهُ أَكْبَرُ كَبِيراً، وَالْحَمْدُ لِلَّهِ كَثِيراً، سُبْحَانَ اللَّهِ رَبِّ العَالَمِينَ، لاَ حَوْلَ وَلاَ قُوَّةَ إِلاَّ بِاللَّهِ الْعَزِيزِ الْحَكِيمِ)) قَالَ: فَهَؤُلاَءِ لِرَبِّي، فَمَا لِي؟ قَالَ: ((قُلْ: اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي، وَارْحَمْنِي، وَاهْدِنِي، وَارْزُقْنِي)).

Alikuja mtu mmoja wa shamba kwa Mtume (s.a.w) akamwambia, nifundishe maneno nitakayo yasema, Mtume (s.a.w) akamwambia: Sema: ''Hapana mola apasae kuabudiwa kwa haki ila ni Mwenyezi Mungu hali ya kuwa peke yake, wala hana mshirika wake, Mwenyezi Mungu ni Mkubwa tena sana, na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu tena nyingi sana, Ametakasika Mwenyezi Mungu Mwenye Kutukuka, Mwingi wa Hekima.'' ......Yule mtu kisha akasema, Haya ni ya Mwenyezi Mungu, ni yapi yangu? Mtume (s.a.w) akamwambia, Sema: ''Ewe Mwenyezi Mungu, nisamehe, na unirehemu, na uniongoze, na uniruzuku.''

Sikiliza · Sauti ya Hamad al-Duraiham

Dhikri · 15 lugha