((لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ وَحْدَهُ لاَ شَرِيكَ لَهُ، لَهُ الْمُلْكُ وَلَهُ الْحَمْدُ، وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ)) (عشرَ مرَّات) ، أَوْ (مرَّةً واحدةً عندَ الكَسَلِ).
Amesema Mtume (s.a.w): Mwenye kusema inapoingia asubuhi: Hapana Mola apasae kuabudiwa kwa haki ila ni Mwenyezi Mungu peke yake, hana mshirika wake, niwake Ufalme, na ni zake sifa njema zote, na Yeye juu ya kila kitu ni Muweza. ......kwa siku mara mia moja, basi yeye ana thawabu za kuwaacha huru watumwa kumi, na ataandikiwa thawabu mia moja, na atafutiwa madhambi mia moja, na atakuwa na kinga ya shetani kwa siku hiyo mpaka jioni, na hapatakuwa na mtu bora kumshinda, ila yule aliyefanya zaidi yake.
Sikiliza · Sauti ya Hamad al-Duraiham