MwanzoDhikriNyiradi za wakati wa kulaladhikri 13

Nyiradi za wakati wa kulala — dhikri 13

أذكار النوم · Hisnul Muslim · 13 / 13

Soma · SikilizaFaili la PDF

((اللَّهُمَّ أَسْلَمْتُ نَفْسِي إِلَيْكَ، وَفَوَّضْتُ أَمْرِي إِلَيْكَ، وَوَجَّهْتُ وَجْهِي إِلَيْكَ، وَأَلْجَأْتُ ظَهْرِي إِلَيْكَ، رَغْبَةً وَرَهْبَةً إِلَيْكَ، لاَ مَلْجَأَ وَلاَ مَنْجَا مِنْكَ إِلاَّ إِلَيْكَ، آمَنْتُ بِكِتَابِكَ الَّذِي أَنْزَلْتَ، وَبِنَبِيِّكَ الَّذِي أَرْسَلْتَ)).

Ukitaka kulala tawadha udhu kama wa swala kisha lalia ubavu wako wa kulia kisha useme: Ewe Mwenyezi Mungu nimeisalimisha nafsi yangu kwako, na nimekuachia mambo yangu Wewe, na nimeuelekeza uso wangu kwako, na nimeutegemeza mgongo wangu kwako, kwa matarajio na kwa kukuogopa, hapana sehemu ya kukimbilia wala ya kujiokoa ila kwako, nimekiamini kitabu chako ulicho kiteremsha, na Mtume wako uliyemtuma. Amesema Mtume (s.a.w) kwa mwenye kuyasema hayo, kisha akafa atakuwa amekufa katika uislamu (kiislamu).

Sikiliza · Sauti ya Hamad al-Duraiham

Dhikri · 15 lugha