MwanzoDhikriDua baada ya tashahhud ya mwisho kabla ya salamdhikri 8

Dua baada ya tashahhud ya mwisho kabla ya salam — dhikri 8

الدعاء بعد التشهد الأخير قبل السلام · Hisnul Muslim · 8 / 11

Soma · SikilizaFaili la PDF

((اللَّهُمَّ بِعِلْمِكَ الغَيْبَ وَقُدْرَتِكَ عَلَى الْخَلقِ أَحْيِنِي مَا عَلِمْتَ الْحَيَاةَ خَيْراً لِي، وَتَوَفَّنِي إِذَا عَلِمْتَ الْوَفَاةَ خَيْراً لِي، اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ خَشْيَتَكَ فِي الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ، وَأَسْأَلُكَ كَلِمَةَ الْحَقِّ فِي الرِّضَا وَالْغَضَبِ، وَأَسْأَلُكَ الْقَصْدَ فِي الْغِنَى وَالْفَقْرِ، وَأَسْأَلُكَ نَعِيماً لاَ يَنْفَدُ، وَأَسْأَلُكَ قُرَّةَ عَيْنٍ لاَ تَنْقَطِعُ، وَأَسْأَلُكَ الرِّضَا بَعْدَ الْقَضَاءِ، وَأَسْــــأَلُكَ بَرْدَ الْعَيْشِ بَعْدَ الْمَوْتِ، وَأَسْأَلُكَ لَذَّةَ النَّظَرِ إِلَى وَجْهِكَ، وَالشَّوْقَ إِلَى لِقائِكَ فِي غَيرِ ضَرَّاءَ مُضِرَّةٍ، وَلاَ فِتْنَةٍ مُضِلَّةٍ، اللَّهُمَّ زَيِّنَا بِزِينَةِ الإِيمَانِ، وَاجْعَلْنَا هُدَاةً مُهْتَدِينَ)).

Ewe Mwenyezi Mungu, kwa ujuzi wako wa mambo yaliyo fichikana, na uwezo wako wa kuumba, niweke iwapo uhai wangu ni bora kwangu, na nifishe iwapo kufa ni bora kwangu, Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi nakuomba khofu yako kwa siri na dhahiri, na ninakuomba neno la haki wakati nimefurahi na wakati nimekasirika, na ninakuomba matumizi ya wastani wakati wa utajiri na wakati wa umasikini, na ninakuomba neema isiyokwisha, na ninakuomba kituliza jicho (moyo) kisicho katika, na ninakuomba kuridhia baada ya kuwa umesha nipangia, na ninakuomba maisha ya utulivu baada ya kufa, na ninakuomba ladha ya kuuona uso wako, na shauku ya kukutana na wewe, pasina madhara yanayodhuru wala fitna yenye kupoteza, Ewe Mwenyezi Mungu, tupambe kwa kipambo cha imani, na tujaalie tuwe waongozi wenye kuongoka.

Sikiliza · Sauti ya Hamad al-Duraiham

Dhikri · 15 lugha