MwanzoDhikriDua za adhanadhikri 2

Dua za adhana — dhikri 2

أذكار الآذان · Hisnul Muslim · 2 / 5

Soma · SikilizaFaili la PDF

يَقُولُ: ((وَأَنَا أَشْهَدُ أَنْ لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ وَحْدَهُ لاَ شَرِيكَ لَهُ وَأَنَّ مُحَمَّداً عَبْدُهُ وَرَسُولُهُ، رَضِيتُ بِاللَّهِ رَبَّاً، وَبِمُحَمَّدٍ رَسُولاً، وَبِالْإِسْلاَمِ دِينَاً)) ((يَقُولُ ذَلِكَ عَقِبَ تَشَهُّدِ الْمُؤَذِّنِ)).

Muadhini akisema: Ash-hadu anlaa ilaha illa Llaah, ash-hadu anna Muhammada Rrasuulu Llaah, anatakiwa mtu aseme: Na mimi pia nakiri kwa moyo na kusema kwa ulimi ya kwamba hapana Mola apasae kuabudiwa kwa haki, isipokuwa Mwenyezi Mungu mmoja peke yake, hana mshirika wake, na kwamba Muhammad ni mja wake, na ni Mtume wake, nimeridhia kuwa Mwenyezi Mungu ndie Mola wangu, na kuwa Muhammad ni Mtume wangu, na kuwa Uislamu ndiyo dini yangu. Anayasema hayo mwisho wa Adhana.

Sikiliza · Sauti ya Hamad al-Duraiham

Dhikri · 15 lugha