MwanzoDhikriNyiradi baada ya kutoa salam (kumaliza swala)dhikri 5

Nyiradi baada ya kutoa salam (kumaliza swala) — dhikri 5

الأذكار بعد السلام من الصلاة · Hisnul Muslim · 5 / 8

Soma · SikilizaFaili la PDF

بسم الله الرحمن الرحيم ﴿قُلْ هُوَ اللَّهُ أَحَدٌ* اللَّهُ الصَّمَدُ* لَمْ يَلِدْ وَلَمْ يُولَدْ* وَلَمْ يَكُن لَّهُ كُفُواً أَحَدٌ﴾، بسم الله الرحمن الرحيم ﴿قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ الْفَلَقِ* مِن شَرِّ مَا خَلَقَ* وَمِن شَرِّ غَاسِقٍ إِذَا وَقَبَ* وَمِن شَرِّ النَّفَّاثَاتِ فِي الْعُقَدِ* وَمِن شَرِّ حَاسِدٍ إِذَا حَسَدَ﴾،بسم الله الرحمن الرحيم ﴿قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ النَّاسِ* مَلِكِ النَّاسِ* إِلَهِ النَّاسِ* مِن شَرِّ الْوَسْوَاسِ الْخَنَّاسِ* الَّذِي يُوَسْوِسُ فِي صُدُورِ النَّاسِ* مِنَ الْجِنَّةِ وَ النَّاسِ﴾ بَعْدَ كُلِّ صَلاَةٍ.

Kwa jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema mwenye kurehemu. {Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa pekee* Mwenyezi Mungu Mkusudiwa* Hakuzaa wala hakuzaliwa* Wala hana anaye fanana naye hata mmoja}. Kwa jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema mwenye kurehemu. {Sema: Najikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko* Na shari ya alivyo viumba* Na shari ya giza la usiku liingiapo* Na shari ya wanao pulizia mafundoni* Na shari ya hasidi anapo husudu}. Kwa jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema mwenye kurehemu. {Sema: Ninajikinga kwa Mola Mlezi wa wanaadamu* Mfalme wa wanaadamu* Mungu wa wanaadamu* Na shari ya wasiwasi wa Shetani, Khannas* Anaye tia wasiwasi katika vifua vya watu* Kutokana na majini na wanaadamu}. Atasoma kila baada ya swala mara moja, na baada ya swala ya Magharibi na Alfajiri atazisoma hizo mara tatu tatu. Pia ni katika Sunnah kusoma Aayatul-Kursiy baada ya kila swala.

Sikiliza · Sauti ya Hamad al-Duraiham

Dhikri · 15 lugha