MwanzoDhikriNyiradi za asubuhi na jionidhikri 3

Nyiradi za asubuhi na jioni — dhikri 3

أذكار الصباح والمساء · Hisnul Muslim · 3 / 24

Soma · SikilizaFaili la PDF

((أَصْبَحْنَا وَأَصْبَحَ الْمُلْكُ لِلَّهِ ، وَالْحَمْدُ لِلَّهِ، لاَ إِلَهَ إلاَّ اللَّهُ وَحْدَهُ لاَ شَرِيكَ لَهُ، لَهُ الْمُلْكُ وَلَهُ الْحَمْدُ وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ، رَبِّ أَسْأَلُكَ خَيْرَ مَا فِي هَذَا الْيَوْمِ وَخَيرَ مَا بَعْدَهُ ، وَأَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ مَا فِي هَذَا الْيَوْمِ وَشَرِّ مَا بَعْدَهُ، رَبِّ أَعُوذُ بِكَ مِنَ الْكَسَلِ وَسُوءِ الْكِبَرِ، رَبِّ أَعُوذُ بِكَ مِنْ عَذَابٍ فِي النَّارِ وَعَذَابٍ فِي الْقَبْرِ)). [ وإذا أمسى قال: أمسينا وأمسى الملك للَّه] [وإذا أمسى قال: رب أسألك خير ما في هذه الليلة، وخير ما بعدها، وأعوذ بك من شر ما في هذه الليلة، وشر ما بعدها.]

Tumeingia wakati wa asubuhi na umekuwa Ufalme ni wa Mwenyezi Mungu, na sifa njema ni za Mwenyezi Mungu, hapana Mola apasae kuabudiwa kwa ila ni Mwenyezi Mungu, hali ya kuwa peke yake hana mshirika, ni wake Ufalme na ni zake sifa njema, na Yeye juu ya kila kitu ni Muweza, Ewe Mola, nakuomba kheri ya siku ya leo, na kheri ya baada ya siku hii, na ninajilinda kwako kutokana na shari ya siku ya leo na shari ya baada ya siku hii, Ewe Mola, najilinda kwako kutokana na uvivu, na ubaya wa uzee (uzee mbaya), Ewe Mola, najilinda kwako kutokana na adhabu ya moto na adhabu ya kaburi. Na ikiingia jioni atasema: Tumeingia jioni na imefika jioni na Ufalme ni wa Mwenyezi Mungu, Mola wa viumbe vyote, Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi nakuomba kheri ya usiku huu, na najilinda kwako kutokana na shari ya kilicho ndani ya usiku huu, na shari ya baada ya usiku huu.

Sikiliza · Sauti ya Hamad al-Duraiham

Dhikri · 15 lugha