((سُبْحَانَ اللَّهِ (ثلاثاً وثلاثين) وَالْحَمْدُ لِلَّهِ (ثلاثاً وثلاثين) وَاللَّهُ أَكْبَرُ (أربعاً وثلاثينَ))).
(106) Mtume (s.a.w) amesema: ''Hivi niwafahamishe juu ya kitu ambacho ni bora zaidi kuliko mtumishi, wakati mnapolala; msabihini Mwenyezi Mungu (kwa kusema Subhana Llaah) mara thelathini na tatu, kisha msifuni Mwenyezi Mungu (kwa kusema Alhamdu liLlaah) mara thelathini na tatu, na kisha mkabirini Mwenyezi Mungu (kwa kusema Allahu akbar) mara thelathini na nne, kwani kusema hivo ni bora kwenu kuliko mtumishi. Yaani useme: Subhaana Llaah, (Ametakasika Mwenyezi Mungu). Mara thelathini na tatu. Wa Alhamdu liLlaah, (Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu). Mara thelathini na tatu. Wa Allaahu akbar, (Mwenyezi Mungu ni mkubwa). Mara thelathini na nne.
Sikiliza · Sauti ya Hamad al-Duraiham